English Kiswahili

Maandalizi ya Makala ya kumbukizi ya Ukoloni, Tanzania

Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma imepata nafasi ya kushiriki kwenye uandaaji wa Makala ya redio ya Shirika la Utangazaji la Ujerumani kuhusu kumbukumbu ya Historia ya kikoloni nchini Tanzania kwa kuangazia namna gani wananchi wanaikumbuka na jitihada za taasisi hususan Makumbusho wanavyoitunza Historia hiyo.

Kulia ni Bwana, Jochen Rack kutoka Shirika la Utangazaji Ujerumani (Bavaria Broadcast Corporation)

Tanzia Mhe. Balozi Dkt. Augustine P. Mahiga

Dkt. Augustine Philip Mahiga, Balozi na Waziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amefariki dunia leo alfajiri 01 Mei, 2020 Jijini Dodoma.

Daima tutakumbuka na tutamenzi Dkt. Mahiga kama Balozi wa fahari yetu kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kama Balozi wa Mkoa wa Iringa na watu wake kwa dunia nzima. Tangu alipofungua rasmi Makumbusho ya Mkoa wa Iringa Boma mwaka 2016, alitushauri na kutuongoza ktk kuendeleza kazi yetu na kuitangaza kitaifa na kimataifa. Tunamwombea kwa Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi. Tunapenda kutoa salamu za rambirambi za dhati kwa familia na ndugu yake pamoja na watu wote walio karibu naye.

Iringa Boma Easter Market 2023

08. Apr 2023 to 09. Apr 2023

Iringa Boma Easter Market

Iringa Boma Easter Market 2022

16. Apr 2022 to 16. Apr 2022

Easter Market Event

Ufunguzi wa maonesho mapya ya “Mabadiliko ya Binadamu”

05. Dec 2020

Maonesho yaliyosubiriwa kwa hamu pamoja na mambo mengi zaidi...

Jhikoman Reggae Jam Session 2 @Iringa Sunset Hotel

01. Oct 2019

Usikose kumwona tena!

Reggae Live: Jhikoman & Afrikabisa Band

25. Sep 2019

Ni kitu kipya Iringa...

Iringa Boma Siku ya Pasaka 2019

20. Apr 2019

Kwa mara nyingine tena...

Iringa Boma Siku ya Makumbusho Duniani

18. May 2018 to 20. May 2018

maonesho mapya...mitazamo mipya...hadhira mpya...

Iringa Boma Easter Special

29. Mar 2018

Jiandae kwa pasaka!

Iringa Boma Usiku wa Wapendanao

14. Feb 2018

A night to remember!

Ufunguzi Iringa Boma-Makumbusho ya Mkoa & Kituo cha Utamaduni

25. Jun 2016

Ni wakati wa Iringa kung'aa! Kile Kituo cha utamaduni na Makumbusho ya mkoa wa Iringa sasa kitafunguliwa rasmi Juni 25 mwaka huu (2016).

International Summer School: Urithi wa Afrika na nguzo endelevu

25. Jul 2016 to 31. Jul 2016

Kuiweka Iringa kwenye ramani ya masomo ya Urithi wa dunia