English Kiswahili

Uzinduzi wa Maonesho Mapya ya Masimulizi ya Kiasili ya Kusisimua.

Makumbusho ya mkoa – Iringa Boma imezindua maonesho mapya ya Masimulizi ya kiasili ya kusisimua yenye lengo la kuhifadhi na kurithisha masimulizi na hadithi zilizopo kwenye hatari ya kupotea kwenye jamii ya sasa.

Maonesho hayo yalizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mkoa Iringa Mh. Queen Cuthbert Sendiga pamoja na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya, Manispaa, Wazee wa kimila na wageni wengine.

 

 

 

Maonesho ya vyuo vikuu Tanzania Mnazi Mmoja

Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma na Mradi wa fahari yetu Tanzania kwa kushirikiana na Chuo kikuu cha Iringa tumepata nafasi ya kushiriki maonesho ya vyuo vikuu Tanzania yanayo fanyika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es salaam. Tupo kwenye banda la Chuo Kikuu Iringa karibu upate kuifahamu historia ya Mkoa wa Iringa kwa ufupi.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa watembelea Makumbusho ya Mkoa

Wiki hii Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma tulipata ugeni wa Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Iringa (Waalimu watalajiwa) wenye lengo la kujifunza Historia ya Iringa na wakazi wake kwa ajili ya kuandika kazi mradi. Makumbusho imekuwa ni kituo cha kujifunza na kuelimisha kuhusu utamaduni wa watu mbalimbali. Tunakaribisha shule, vyuo na taasisi za kiserikali na zile binafsi kwa ajili ya kujifunza tamaduni na historia ya Iringa.

 

Iringa Boma Easter Market 2023

08. Apr 2023 to 09. Apr 2023

Iringa Boma Easter Market

Iringa Boma Easter Market 2022

16. Apr 2022 to 16. Apr 2022

Easter Market Event

Ufunguzi wa maonesho mapya ya “Mabadiliko ya Binadamu”

05. Dec 2020

Maonesho yaliyosubiriwa kwa hamu pamoja na mambo mengi zaidi...

Jhikoman Reggae Jam Session 2 @Iringa Sunset Hotel

01. Oct 2019

Usikose kumwona tena!

Reggae Live: Jhikoman & Afrikabisa Band

25. Sep 2019

Ni kitu kipya Iringa...

Iringa Boma Siku ya Pasaka 2019

20. Apr 2019

Kwa mara nyingine tena...

Iringa Boma Siku ya Makumbusho Duniani

18. May 2018 to 20. May 2018

maonesho mapya...mitazamo mipya...hadhira mpya...

Iringa Boma Easter Special

29. Mar 2018

Jiandae kwa pasaka!

Iringa Boma Usiku wa Wapendanao

14. Feb 2018

A night to remember!

Ufunguzi Iringa Boma-Makumbusho ya Mkoa & Kituo cha Utamaduni

25. Jun 2016

Ni wakati wa Iringa kung'aa! Kile Kituo cha utamaduni na Makumbusho ya mkoa wa Iringa sasa kitafunguliwa rasmi Juni 25 mwaka huu (2016).

International Summer School: Urithi wa Afrika na nguzo endelevu

25. Jul 2016 to 31. Jul 2016

Kuiweka Iringa kwenye ramani ya masomo ya Urithi wa dunia