Wiki hii Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma tulipata ugeni wa Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Iringa (Waalimu watalajiwa) wenye lengo la kujifunza Historia ya Iringa na wakazi wake kwa ajili ya kuandika kazi mradi. Makumbusho imekuwa ni kituo cha kujifunza na kuelimisha kuhusu utamaduni wa watu mbalimbali. Tunakaribisha shule, vyuo na taasisi za kiserikali na zile binafsi kwa ajili ya kujifunza tamaduni na historia ya Iringa.