Kila kitu hewani!
Bonyeza hapa:
Proceedings: African Heritage and the Pillars of Sustainability
Kwa Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Iringa!
Usikose nafasi hii nzuri ikiwa wewe ni mmoja wa walengwa wafuatayo:
Don’t miss this great opportunity if you belong the the following target groups:
Fanya maombi kabla ya tarehe 21/11/2016 ili kushiriki muhula wa pili 2016/2017 katika Chuo cha Göttingen, Ujerumani
Angalia taarifa zote kuhusu kutuma maombi:
Nafasi hii inafadhiliwa na Jumuiya ya Umoja wa Ulaya kupitia Erasmus+ KA 107 (Mobility with Partner Countries): Go International Plus 2016 programme.
Katika juma la ufunguzi wa Makumbusho ya Mkoa – Iringa Boma, tulimkaribisha mwanasanaa Hans Poppe, kutoka Canada ambaye familia yake ina asili ya Iringa. Michoro yake yenye ufanisi wa Kiswahili iliongeza thamani kubwa katika ufunguzi huu. Wanajamii walipata nafasi ya kukutana na msanii pamoja na matembezi katika Makumbusho. Miongoni mwa kazi hizi za sanaa zitaendelea kubaki katika Makumbusho.
Shukrani za dhati ziende kwa Hans na wote walioshiriki kukamilisha maonesho haya.
Picha na Darlene Parker na Hans Poppe
Karibu kutembelea Makumbusho!
Kila siku Makumbusho itafunguliwa kuanzia saa 3:30 asubuhi mpaka saa 12:00.
Makumbusho inapatikana katikati mwa Mji wa Iringa. Hapa ni sehemu sahihi kwa ajili ya taarifa za nyakati tofauti za Hitoria ya Iringa, wakazi wake na tamaduni zao pamoja na sehemu za kusisimua zenye kuufanya upekee wa Iringa.
Pamoja na maonesho ya muda kuna taarifa za Historia ya Iringa na Tunu za Asili na Kitamaduni basi kuna cha kumvutia kila mmoja anayeweza kufika.
Grarama za kiingilio
Wakubwa – Wasio na Kibadli cha kuishi Nchini – Shilingi 10,000
Wanafunzi – Wasion na Kibali cha kuishi Nchini – Shilingi 5,000
Wageni wenye vibali vya kuishi Nchini – Shilingi 5,000
Watanzania Wakubwa – Shilingi 3,000
Watanzania wanafunzi – Shilingi 1,000
Mwaka 2014, mradi wa fahari yetu ulianza kazi kubwa ya kukarabati Boma la wajerumani. Jengo hili liliachwa wazi na ofisi ya mkuu wa wilaya iliyokuwa ikilitumia kabla ya fahari yetu kuanza ukarabati. Moja ya malengo makuu ya mradi ni kutunza, kukuza, kutoa mwamko na kujivunia utamaduni. Kubadilishana na kushiriki kwa kuonesha masuala ya kitamaduni na kushirikisha umma.
Baada ya kukamilika kwa ukarabati wa Boma, ambalo sasa ni makumbusho ya Mkoa na kituo cha utamaduni, siku ya Jumamosi Juni 25, 2016, makumbusho yatafunguliwa kwa umma. Sherehe rasmi za ufunguzi zitafanyika siku hiyo kwa kushirikiana na wadau, wafuasi, washirika, wafadhili na wawakilishi wa serikali.
Ratiba kamili ya matukio ya siku hiyo itawekwa hapa katika wiki zijazo, hivyo tafadhali endelea kupitia tovuti yetu, lakini pia usisahau kuongeza tukio hili katika kalenda yako….It’s Iringa’s time to shine!
14. Feb 2018