English Kiswahili

Maombi ya masomo ya kubadilishana Muhula Ujerumani

Kwa Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Iringa!

Usikose nafasi hii nzuri ikiwa wewe ni mmoja wa walengwa wafuatayo:

Don’t miss this great opportunity if you belong the the following target groups:

  1. Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamili ya Sanaa katika Utalii, Utamaduni na Jamii (Master of Arts in Tourism, Culture and Society – MATCS)
  2. Wafanyakazi wa Kiakademia kutoka idara ya Anthropolojia ya Utamaduni na Utalii na idara nyingine zenye utafiti ya kijamii na zilizo na utamaduni au nia ya kufundisha.

Fanya maombi kabla ya tarehe 21/11/2016 ili kushiriki muhula wa pili 2016/2017 katika Chuo cha Göttingen, Ujerumani

Angalia taarifa zote kuhusu kutuma maombi:

Nafasi hii inafadhiliwa na  Jumuiya ya Umoja wa Ulaya kupitia Erasmus+ KA 107 (Mobility with Partner Countries): Go International Plus 2016 programme.

uoi_logo_modified_v2_uoi                                                                                                          ugoe-logo

 

Maonesho ya Sanaa ya kukumbukwa

boma art exhibit boma art exhibit

Katika juma la ufunguzi wa Makumbusho ya Mkoa – Iringa Boma, tulimkaribisha mwanasanaa Hans Poppe, kutoka Canada ambaye familia yake ina asili ya Iringa. Michoro yake yenye ufanisi wa Kiswahili iliongeza thamani kubwa katika ufunguzi huu. Wanajamii walipata nafasi ya kukutana na msanii pamoja na matembezi katika Makumbusho. Miongoni mwa kazi hizi za sanaa zitaendelea kubaki katika Makumbusho.

Shukrani za dhati ziende kwa Hans na wote walioshiriki kukamilisha maonesho haya.

hans2 hans3

Picha na Darlene Parker na Hans Poppe

 

Makumbusho ya Mkoa – Iringa Boma yafunguliwa rasmi!!

Karibu kutembelea Makumbusho!

Kila siku Makumbusho itafunguliwa kuanzia saa 3:30 asubuhi mpaka saa 12:00.

Makumbusho inapatikana katikati mwa Mji wa Iringa. Hapa ni sehemu sahihi kwa ajili ya taarifa za nyakati tofauti za Hitoria ya Iringa, wakazi wake na tamaduni zao pamoja na sehemu za kusisimua zenye kuufanya upekee wa Iringa.

Irinaa Boma Museum
Karibu Makumbusho ya Mkoa – Iringa Boma

Pamoja na maonesho ya muda kuna taarifa za Historia ya Iringa na Tunu za Asili na Kitamaduni basi kuna cha kumvutia kila mmoja anayeweza kufika.

Grarama za kiingilio

Wakubwa – Wasio na Kibadli cha kuishi Nchini    – Shilingi 10,000

Wanafunzi – Wasion na Kibali cha kuishi Nchini   – Shilingi 5,000

Wageni wenye vibali vya kuishi Nchini                 – Shilingi 5,000

Watanzania Wakubwa                                          – Shilingi 3,000

Watanzania wanafunzi                                         – Shilingi 1,000

boma museum boma museum boma museum IMG_8007

Uzinduzi wa Iringa Boma-Makumbusho ya Mkoa na Kituo cha Utamaduni

Mwaka 2014, mradi wa fahari yetu ulianza kazi kubwa ya kukarabati Boma la wajerumani. Jengo hili liliachwa wazi na ofisi ya mkuu wa wilaya iliyokuwa ikilitumia kabla ya fahari yetu kuanza ukarabati. Moja ya malengo makuu ya mradi ni kutunza, kukuza, kutoa mwamko na kujivunia utamaduni. Kubadilishana na kushiriki kwa kuonesha masuala ya kitamaduni na kushirikisha umma.

Iringa Boma 2014
Boma prior to renovation in 2014

 

Baada ya kukamilika kwa ukarabati wa Boma, ambalo sasa ni makumbusho ya Mkoa na kituo cha utamaduni, siku ya Jumamosi Juni 25, 2016,  makumbusho yatafunguliwa kwa umma. Sherehe rasmi za ufunguzi zitafanyika siku hiyo kwa kushirikiana na wadau, wafuasi, washirika, wafadhili na wawakilishi wa serikali.

Iringa Boma 2016
The renovated Boma 2016

 

Ratiba kamili ya matukio ya siku hiyo itawekwa hapa katika wiki zijazo, hivyo tafadhali endelea kupitia tovuti yetu, lakini pia usisahau kuongeza tukio hili katika kalenda yako….It’s Iringa’s time to shine!

Iringa Boma Easter Market 2023

08. Apr 2023 to 09. Apr 2023

Iringa Boma Easter Market

Iringa Boma Easter Market 2022

16. Apr 2022 to 16. Apr 2022

Easter Market Event

Ufunguzi wa maonesho mapya ya “Mabadiliko ya Binadamu”

05. Dec 2020

Maonesho yaliyosubiriwa kwa hamu pamoja na mambo mengi zaidi...

Jhikoman Reggae Jam Session 2 @Iringa Sunset Hotel

01. Oct 2019

Usikose kumwona tena!

Reggae Live: Jhikoman & Afrikabisa Band

25. Sep 2019

Ni kitu kipya Iringa...

Iringa Boma Siku ya Pasaka 2019

20. Apr 2019

Kwa mara nyingine tena...

Iringa Boma Siku ya Makumbusho Duniani

18. May 2018 to 20. May 2018

maonesho mapya...mitazamo mipya...hadhira mpya...

Iringa Boma Easter Special

29. Mar 2018

Jiandae kwa pasaka!

Iringa Boma Usiku wa Wapendanao

14. Feb 2018

A night to remember!

Ufunguzi Iringa Boma-Makumbusho ya Mkoa & Kituo cha Utamaduni

25. Jun 2016

Ni wakati wa Iringa kung'aa! Kile Kituo cha utamaduni na Makumbusho ya mkoa wa Iringa sasa kitafunguliwa rasmi Juni 25 mwaka huu (2016).

International Summer School: Urithi wa Afrika na nguzo endelevu

25. Jul 2016 to 31. Jul 2016

Kuiweka Iringa kwenye ramani ya masomo ya Urithi wa dunia