Makumbusho ya mkoa – Iringa Boma imezindua maonesho mapya ya Masimulizi ya kiasili ya kusisimua yenye lengo la kuhifadhi na kurithisha masimulizi na hadithi zilizopo kwenye hatari ya kupotea kwenye jamii ya sasa.

Maonesho hayo yalizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mkoa Iringa Mh. Queen Cuthbert Sendiga pamoja na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya, Manispaa, Wazee wa kimila na wageni wengine.