Mnamo tarehe 5 mwezi wa 12, maonesho mapya yanayoelezea chimbuko na mabadiliko ya Binadamu yamefunguliwa rasmi na Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma. Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Tanzania na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa walihudhuria. Hafla ya ufunguzi iliambatana na burudani mpaka saa nne na nusu usiku.