Uzinduzi wa Maonesho Mapya ya Masimulizi ya Kiasili ya Kusisimua.

Makumbusho ya mkoa – Iringa Boma imezindua maonesho mapya ya Masimulizi ya kiasili ya kusisimua yenye lengo la kuhifadhi na kurithisha masimulizi na hadithi zilizopo kwenye hatari ya kupotea kwenye jamii ya sasa.

Maonesho hayo yalizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mkoa Iringa Mh. Queen Cuthbert Sendiga pamoja na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya, Manispaa, Wazee wa kimila na wageni wengine.

 

 

 

Maonesho ya vyuo vikuu Tanzania Mnazi Mmoja

Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma na Mradi wa fahari yetu Tanzania kwa kushirikiana na Chuo kikuu cha Iringa tumepata nafasi ya kushiriki maonesho ya vyuo vikuu Tanzania yanayo fanyika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es salaam. Tupo kwenye banda la Chuo Kikuu Iringa karibu upate kuifahamu historia ya Mkoa wa Iringa kwa ufupi.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa watembelea Makumbusho ya Mkoa

Wiki hii Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma tulipata ugeni wa Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Iringa (Waalimu watalajiwa) wenye lengo la kujifunza Historia ya Iringa na wakazi wake kwa ajili ya kuandika kazi mradi. Makumbusho imekuwa ni kituo cha kujifunza na kuelimisha kuhusu utamaduni wa watu mbalimbali. Tunakaribisha shule, vyuo na taasisi za kiserikali na zile binafsi kwa ajili ya kujifunza tamaduni na historia ya Iringa.