Kumbukizi ya Mashujaa Walio Pigana Vita ya Majimaji Songea

Mwaka 2023 imetimu miaka  116  tangu kumalizika kwa vita vya majimaji vilivyodumu kuanzia mwaka 1905  hadi 1907 vikihusisha makabila mbalimbali kutoka kusini kwa Tanganyika walioungana chini ya kiongozi wao kinjekitile ngwale  kupinga utawala wa kikoloni wa kijerumani, katika mapigano hayo inakadiriwa Zaidi ya watu alfu 75 mpaka laki tatu walipoteza Maisha kutokana na njaa, magonjwa na unyanyasaji , huku askari kijerumani waliibuka washindi katika uwanja wa mapambano..

Kwa kutambua mchango wa wapambanaji waliopoteza Maisha katika vita hiyo wizara ya utalii Tanzania  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa utalii nchini waliandaa tamasha maalumu kwaajili ya maonesho ya sehemu mbalimbali nchini na mkoa wa Ruvuma ambapo Mgeni rasmi alikuwa naibu Waziri wa maliasilli na utalii Tanzania Mhe.Marry Masanja Pamoja nakuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kidini na serikali.

Katika madhimisho hayo Mradi wa fahari yetu Tanzania na makumbusho ya mkoa Iringa Boma tulipata nafasi ya kushiriki katika maadhimisho ya miaka 116 tangu kumalizika kwa vita hiyo , kwa lengo la kujifunzana kudumisha ushirikiano na wadau mbalimbali wa utalii nchini Tanzania..

Ziara ya Mkuregenzi wa Mradi wa fahari yetu Tanzania Jijini Dar es salaam

Mkurugenzi wa fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya Mkoa Iringa – Boma Dk. Jan Kuver akiwa kwenye ziara yake Jijini Dar es salaam alitembelea makumbusho ya Taifa ya Tanzania na kukutana na Mkurugenzi wa makumbusho hiyo Dk. Noel Lwoga.

Kuimalisha mahusiano baina ya makumbusho ya Taifa na Makumbusho zilizo chini ya Taasisi binafsi nimoja kati ya vitu walivyokubaliana wakati wa mazungumzo. Hata hivyo Dk. Noel ameeleza ya kuwa wataitumia siku ya Makumbusho Duniani ambayo huu adhimishwa tarehe 18 mwezi Mei kwa lengo la kukutana na wadau pamoja na Viongozi mbalimbali wa Makumbusho ili kubadilishana uzoefu na kujadili mwelekeo wa sekta ya utalii wa Mambo kale.

 

 

Maonesho ya Karibu Kusini 2022

Umepita miaka miwili tangu kuaharishwa kwa tamasha la karibu kusini kutokana na kuwepo kwa janga la Uviko 19 Tanzania na Duniani kwa Ujumla. Mwaka 2022 kumekuwana athari ndogo zinazo sababishwa na Janga la Uviko-19 hivyokupeleka kufanyika kwa Tamasha la Karibu Kusini mkoani Iringa.

Tamasha na maonesho ya karibu kusini yenye lengo la kutangaza utalii uliopo kusini mwa Tanzania limefanyika rasmi kwa siku tano mfululizo Mkoani Iringa katika viwanja wa Kihesa kilolo ambapo maonesho hayo yalifunguliwa rasmi na Mhe.balozi Pindi Chana Waziri wa Maliasili na Utalii Tanzania na kudhuriwa na wa kuu wa mikoa mbalimbali, wakuu wa wilaya, Meya, Viongozi wa kisrikali pamoja na wadau wa Utalii.

Wakati wa uzinduzi rasmi Waziri Pindi Chana amesema kuwa lengo la wiazara ya maliasili na utalii ni kuhakikisha wanapata watalii Milioni Tano na Dollar Millioni mia Tano za Kimarekani kupitia uatalii kusini mwa Tanzania hadi kufikia mwaka 2025.

Madhimisho hayo yalifungwa rasmi siku ya Ijuma na Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibari Mhe Othman Masoud Othman ambeye alikubari kuwa balozi wa Utalii kusini mwa Tanzania kwa hiari na kuahidi kutangaza vivutio vinavyopatikana kusini kupitia lango la utalii lililopo Zanzibari.

Maonesho hayo yaliikutanisha mikoa kumi ianayo patikana kusini mwa Tanzania ikiwemo mkoa wa Mtwara,Njombe,Mbeya,Ruvuma,Iringa,Songwe nk.

Mradi wa fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya Mkoa Iringa – Boma tulipata nafasi ya kuonesha kazi zetu na kutangaza makumbusho ya mkoa kama ilivyo kawaida ya maonesho mengine asanteni sana kwa mliofika kutebelea banda letu na kufika katika Makumbusho yetu.

Maonesho ya Vyakula na Vinywaji Asili

Kama ilivyo kawaida ya makumbushoya mkoa Iringa-Boma kila baada ya miezi mitatu hufanya tukio Fulani lenye kuelimisha au kuenzi utamaduni mwaka 2022 kulifanyika maonesho ya vyakula asili katika makumbusho ya mkoa Iringa Boma ikiwa ni kwa mara ya kwnza tangu kuanzishwa makumbusho hii.

Lengo kubwa la kufanya maonesho ya vyakula asili ilikuwa ni kuenzi, kukumbusha na kuelimisha watu kuhusu vyakula vyetu vya asili, kwani katika maonesho hayo watu walipata kujifunza namna kuandaa vyakula hivyo kuanzia hatua ya awali hadi ya mwisho lakini pia watu wote walipata nafasi ya kuonja vyakula na vinywaji hivyo vya asili.

Viazi vitamu , Ugali, Mkande, ni baadhi ya vyakula ambavyo vilikuwepo Ulanzi Msabe na matunda mbalimbali ya Asili yanayopatikana nyanda za juu kusini.

Makumbusho ya Mkoa na Mradi wa fahari yetu Tanzania tunatoa shukrani zetu za dhati kwa wale wote waliofanikiwa kufakia na kufanikisha tukio hili tunawakaribisha tena katika matukio mengine yanayo fuata.

Swahili International Expo (S!TE2022).

SiTE ni moja ya tamasha makubwa lilnalofanyika nchini Tanzania kila mwaka kwa lengo la kutangaza utalii wa ndani na kutafuta wa wekezaji wapya kwenye sekta ya utalii na hata nnje ya utalii, Kwa mara ya sita sasa Tamasha hili limefanyika Nchini tangu kuanzishwa kwake.

Mwaka 2022 Tamasha hili limefanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es laam ikiwa ni miaka miwili imepita bila kuwepo kwa Tamasha hili nchini kwa sababu za Uviko-19. Mradi wa fahari yetu Tanzania na Mkaumbusho ya mkoa Iringa tulipata nafasi ya kuhudhuria  kuonesha, kutangaza na kueleza watu malengo ya Mradi.

Mhe.Dk, Philip Mpango Makumu wa rais wa Nchini Tanzania alikuwa mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa Tamasha la  swahili international expo 2022, sambamba na waziri wa Utalii, naibu waziri wa utalii wabunge, wakuu wa wilaya na mikoa ni miongoni mwa watu walio hudhuria katika maonesho hayo.