Maadhimisho ya Siku ya Chuo Kikuu cha Iringa

 

Chuo kikuu cha Iringa kilifanya maadhimisho yake kwasiku mbili mfululizo tarehe 13.7 Na tarehe 14.7.2022. Maadhimisho hayo yalitanguliwa na maandamano yaliyoanza siku ya kwanza katika viwanja vya Chuo kikuu cha Iringa nakufika katika Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma, ambapo walimu, wanafunzi na wafanyakazi wa Chuo walipokelewa na Makamu Mkuu wa chuo Prof. Ndelilio Urio katika Makumbusho, kisha kutembezwa  nakupewa masimulizi na wafanya kazi wa makumbusho.

Kilele cha siku ya chuo Kiuu cha Iringa kilitamatishwa siku ya pili katika viwanja vya chuo ambapo Mgeni rasmi wa maadhimisho alikuwa ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa. Adolf Mkenda pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa sambamba na wageni wengine.

Chuo kikuu cha Iringa ni moja kati ya wadau wakubwa wa makumbusho ya Mkoa Iringa kama ilivyo elezwa kwa undani kupitia tovuti yetu ya fahari yetu Tanzani.

Maonesho ya siku ya Sabasaba (77) Mkwawa

 

Makumbusho ya mkoa Iringa Boma na Mradi wa fahari yetu Tanzania tulipata nafasi ya kushiriki katika maonesho ya sababa yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo kikuu kishiriki cha Dar es laam Mkwawa, Maonesho hayo yalifunguliwa na Mgeni rasmi Mh.Saad Mtambule Mkuu wa wilaya ya Mufindi Iringa.

Banda la makumbusho ya mkoa Iringa Boma tulipata nafasi ya kutembelewa na Mgeni rasmi wa maonesho haya yaliyofanyika siku ya sabasaba kamailivyo fanyika kwa mabanda mengine, Kutangaza vivutio vya ndani na historia yetu kama watanzania ni moja kati ya vitu alivyo sisitiza mgeni rasmi katika maonesho haya pindi alipo tembelea banda letu.

“Watu wengi wanajua kuwa utalii ni kwenda Mbugani au kupanda mlima Kilimanjaro na kufika katika maeneo ya fukwe, hapana utalii ni Zaidi ya hivi Iringa boma nimependa juhudi zenu katika kutanga utalii wa malekale na historia  lakini tusiishie hap ana tuongeze kasi katika kutangaza utalii huu duniani kote”.

Sikukuu ya sababa illianza rasmi mwaka 1954 tarehe 7 ya mwezi wa 7 baada ya chama cha   TANGANYIKA AFRICAN ASSOCIATION (TAA) na AFRICAN ASSOCIATION (AA) kuungana na kupatikana chama cha TANGANYIKA AFRICAN NATIONAL UNION  (TANU), chama ambacho kili saidia katika kudai uhuru wa Nchi yaTanganyika (1960) chini ya mwalimu Nyerere rais wa kwanza wa Tanganyika.

Kwa kuwa sera ya chama hiki ilikuwa ni Kilimo “Kilimo nii utii wa Mgongo” basi watu wengi waliamua kujihusisha na shughuli za kilimo na walipeleka mazao yao kila siku katika maonesho  yakikuwa yakifanyika siku ya tarehe 7 Mwezi wa 7 ilikuenzi muungano huo, kwa hivi sasa sikuku hii ya wakulima imegeuka na kuwa kama siku ya wafanyabiashara.

Ukumbi wa Siasa ni Kilimo ulipo Iringa mjini ni moja kati ya mazao ya sera ya kilimo iliyoanzishwa miaka ya 1954 baada ya kuzaliwa kwa chama cha TANU.

 

 

 

 

Matembezi ya Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa

Wakati kaitka picha ni Mkurugenzi wa makumbusho ya Taifa Dr. Noel Lwoga alipata nafasi ya kutembelea Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma wakatiakipita Iringa kuelekea Dodoma. Uhifadhi wa malikale kama sehemu ya makumbusho na kituo cha utamaduni na  Masimulizi / historia za wenyeji na Machifu kwa wageni hata wazawa wa Mkoa wa Iringa ni moja ya Juhudi alizo ziunga Mkono wakati wa matembezi.

Pia amepongeza juhudi zinazofanywa na mradi wa fahari yetu Tanzania katika kukuza na kuendeleza utamaduni nyanda zajuu kusini na Tanzania.

 

Iringa Boma Easter Market Event

Ni takribani miaka mi tatu ilipita bila kufanikisha tukio la Easter market katika viwanja vya makumbusho, sababu kubwa ilikuwa Ni ugonjwa wa Uviko 19 uliopelekea kupigwamarufuku kwa mikusanjiko ya watu, mikutano na shughuli mbalimbali zenyeuhitaji wa watu wengi.

Mwaka 2022 umekuwa mwaka wenye bahati kwakufanikiwa kufanya Event hii iliombatana na uzinduzi wa mgahawa wetu Aroma Coffee House @boma, licha ya tukio kupita lakini Mgahawa umeanza kufanya kazi rasmi.

Uongozi wa fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma unatoa shukrani zake za dhati kwa wote walio fanikisha kufanyika kwa tukio hili na wale walio hudhulia siku ya tukio. Uongozi wa mradi unawakaribisha tena kwenye matukio mengine yatakayokuwa yanaendelea, kwani mwisho wa tukio moja ndio mwanzo wa matukio mengine.

Utafiti Mkoa wa Mtwara

Hapo zamani mfumo wa utawala wa kikoloni uliigawa Tanganyika (Tanzania) kwenye majimbo makubwa nane (8), Jimbo la Kusini ambalo lilijumuisha Mikoa ya Ruvuma,Lindi, na Mtwara amabapo makao makuu yalikuwa lindi.

Mwaka 1971 ndipo ulipo anzishwa Mkoa wa Mtwara, kuanzishwa kwa  Mkoa huu kulitokakana na mpango wa Madaraka Mikoani ulio simamiwa na Rais wakwanza wa Tanzania Mwl.Julius.K. Nyerere uliokuwa na lengo la kusogeza huduma kwa wananchi.Tafsiri ya neno “NTWARA” ambalo kwasasa ni Mtwara linatokana na neno la kimakonde “kutwara” lenye maana ya ku-twaaliwa (kuvamiwa na kuchukuliwa mateka).

Asilimia 75 ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara ni Wamakonde.  Wayao na Wamakua miongoni mwa makabila yanayo patikana katika mkoa huu. Mradi fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma tulifanikiwa kufika Mtwara kwa lengo la utafiti, Mikindani,Mtwara mjini, Tandahimba na Newala ni baadhi ya maeneo tuliofanikiwa kufika wakati wautafiti.