Ni takribani miaka mi tatu ilipita bila kufanikisha tukio la Easter market katika viwanja vya makumbusho, sababu kubwa ilikuwa Ni ugonjwa wa Uviko 19 uliopelekea kupigwamarufuku kwa mikusanjiko ya watu, mikutano na shughuli mbalimbali zenyeuhitaji wa watu wengi.

Mwaka 2022 umekuwa mwaka wenye bahati kwakufanikiwa kufanya Event hii iliombatana na uzinduzi wa mgahawa wetu Aroma Coffee House @boma, licha ya tukio kupita lakini Mgahawa umeanza kufanya kazi rasmi.

Uongozi wa fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma unatoa shukrani zake za dhati kwa wote walio fanikisha kufanyika kwa tukio hili na wale walio hudhulia siku ya tukio. Uongozi wa mradi unawakaribisha tena kwenye matukio mengine yatakayokuwa yanaendelea, kwani mwisho wa tukio moja ndio mwanzo wa matukio mengine.