Makumbusho ya mkoa Iringa Boma na Mradi wa fahari yetu Tanzania tulipata nafasi ya kushiriki katika maonesho ya sababa yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo kikuu kishiriki cha Dar es laam Mkwawa, Maonesho hayo yalifunguliwa na Mgeni rasmi Mh.Saad Mtambule Mkuu wa wilaya ya Mufindi Iringa.

Banda la makumbusho ya mkoa Iringa Boma tulipata nafasi ya kutembelewa na Mgeni rasmi wa maonesho haya yaliyofanyika siku ya sabasaba kamailivyo fanyika kwa mabanda mengine, Kutangaza vivutio vya ndani na historia yetu kama watanzania ni moja kati ya vitu alivyo sisitiza mgeni rasmi katika maonesho haya pindi alipo tembelea banda letu.

“Watu wengi wanajua kuwa utalii ni kwenda Mbugani au kupanda mlima Kilimanjaro na kufika katika maeneo ya fukwe, hapana utalii ni Zaidi ya hivi Iringa boma nimependa juhudi zenu katika kutanga utalii wa malekale na historia  lakini tusiishie hap ana tuongeze kasi katika kutangaza utalii huu duniani kote”.

Sikukuu ya sababa illianza rasmi mwaka 1954 tarehe 7 ya mwezi wa 7 baada ya chama cha   TANGANYIKA AFRICAN ASSOCIATION (TAA) na AFRICAN ASSOCIATION (AA) kuungana na kupatikana chama cha TANGANYIKA AFRICAN NATIONAL UNION  (TANU), chama ambacho kili saidia katika kudai uhuru wa Nchi yaTanganyika (1960) chini ya mwalimu Nyerere rais wa kwanza wa Tanganyika.

Kwa kuwa sera ya chama hiki ilikuwa ni Kilimo “Kilimo nii utii wa Mgongo” basi watu wengi waliamua kujihusisha na shughuli za kilimo na walipeleka mazao yao kila siku katika maonesho  yakikuwa yakifanyika siku ya tarehe 7 Mwezi wa 7 ilikuenzi muungano huo, kwa hivi sasa sikuku hii ya wakulima imegeuka na kuwa kama siku ya wafanyabiashara.

Ukumbi wa Siasa ni Kilimo ulipo Iringa mjini ni moja kati ya mazao ya sera ya kilimo iliyoanzishwa miaka ya 1954 baada ya kuzaliwa kwa chama cha TANU.