Maonesho ya pamoja ya Mradi wafahari yetu Tanzania na Kibubu Ufinyanzi yamefanyika kwa mafanikio makubwa katika viwanja vya Nafasi Art Space Mikocheni B jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Januari 2024. Mradi wa wafahari yetu Tanzania uliwasilisha maonesho ya “Endangered Story of Enchanted Place Phase II, huku Kibubu Ufinyanzi wakionyesha ubunifu wao katika kufinyanga vitu vyenye naumbo mbalimbali kwamatumizi ya  kuhifadhi fedha..

Maonesho haya yalikuwa ni matokeo ya ufadhili ambao waliipokea kutoka Nafasi Art Space mwaka mmoja uliopita. Dkt. Noel Lwoga, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maonesho haya, alitoa maoni yake akisema, “Ni vyema kutangaza utalii kwa njia tofauti”. Tumeona mradi wa wafahari Yetu Tanzania wameamua kuleta simulizi zilizomo katika jamii zetu. Simulizi hizi zenye kuibua hisia kwa watu, ingawa zinaweza kuonekana kama za kufikirika lakini nisimulizi zakweli na zenye kusisimua.

Mkurugenzi wa Nafasi Art Space aliongezea kwa kusema kuwa wamefurahi kuona mafanikio ya ufadhili waliotoa na kuwakaribisha wanasanaa wengine kuomba ufadhili. Hama hivyo. Dkt. Jan Kuver, Meneja wa mradi wa fahari yetu Tanzania, alielezea kuwa maonesho haya yalikuwa ya pili, baada ya yale yaawali kufanyika Iringa na sasa yamehamishiwa Dar es Salaam. Pia, wanaendelea kuandaa vitabu vyenye picha za kuchora kwa ajili ya kusambaza mashuleni ili kuendelea kuhifazi msimulizi haya kupitia kwa watoto.

Maonesho haya yamekuwa ni fursa nzuri ya kukuza utamaduni, ubunifu, na kuelimisha jamii kuhusu mambo mbalimbali yanayowahusu. Tunatarajia kuona juhudi kama hizi zikiendelea na kuchochea maendeleo katika sekta za utalii na sanaa nchini Tanzania.

Maonesho ya pamoja ya Mradi wafahari yetu Tanzania na Kibubu Ufinyanzi yamefanyika kwa mafanikio makubwa katika viwanja vya Nafasi Art Space Mikocheni B jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Januari 2024. Mradi wa wafahari yetu Tanzania uliwasilisha maonesho ya “Endangered Story of Enchanted Place Phase II, huku Kibubu Ufinyanzi wakionyesha ubunifu wao katika kufinyanga vitu vyenye naumbo mbalimbali kwamatumizi ya  kuhifadhi fedha..

Maonesho haya yalikuwa ni matokeo ya ufadhili ambao waliipokea kutoka Nafasi Art Space mwaka mmoja uliopita. Dkt. Noel Lwoga, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maonesho haya, alitoa maoni yake akisema, “Ni vyema kutangaza utalii kwa njia tofauti”. Tumeona mradi wa wafahari Yetu Tanzania wameamua kuleta simulizi zilizomo katika jamii zetu. Simulizi hizi zenye kuibua hisia kwa watu, ingawa zinaweza kuonekana kama za kufikirika lakini nisimulizi zakweli na zenye kusisimua.

Mkurugenzi wa Nafasi Art Space aliongezea kwa kusema kuwa wamefurahi kuona mafanikio ya ufadhili waliotoa na kuwakaribisha wanasanaa wengine kuomba ufadhili. Hama hivyo. Dkt. Jan Kuver, Meneja wa mradi wa fahari yetu Tanzania, alielezea kuwa maonesho haya yalikuwa ya pili, baada ya yale yaawali kufanyika Iringa na sasa yamehamishiwa Dar es Salaam. Pia, wanaendelea kuandaa vitabu vyenye picha za kuchora kwa ajili ya kusambaza mashuleni ili kuendelea kuhifazi msimulizi haya kupitia kwa watoto.

Maonesho haya yamekuwa ni fursa nzuri ya kukuza utamaduni, ubunifu, na kuelimisha jamii kuhusu mambo mbalimbali yanayowahusu. Tunatarajia kuona juhudi kama hizi zikiendelea na kuchochea maendeleo katika sekta za utalii na sanaa nchini Tanzania.