Mkoa, kupitia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inatoa msaada wa kiutawala, na pia ni kiungo kati ya serikali kuu na serikali za mitaa. Chombo hiki pia kinachukua jukumu katika kufanikisha ushirikiano kati ya mradi na umma na kutoa misaada ya kiutawala kama vile kuwezesha kufikika kwa maeneo yaliyo katika mradi,kutoa vibali na maeneo kwa ajili ya mradi, kusaidia mradi na vizuizi vya kisiasa, kuandaa matamasha na matukio mengine ya utamaduni