Mgeni rasmi Chifu Joel Mwakatumbula akitoa pongezi zake za dhati kwa mhifadhi mkuu wa makumbusho ya Mkoa Iringa Boma mara baada ya kutembelea banda letu la maonesho siku ya Mpalano Festival.

Mpalano nineno kutoka kabila la Kinyakiyusa, kabila maarufu Mkoani Mbeya, neno Mpalano tafsiri yake ni tujumuike kwa Pamoja neno hili limetumika katika kuanda maonesho yenye tija kwa nyanda za Juu Kusini na yenye lengo la kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nyanda za Juu kusini.

Mradi wa fahari yetu Tanzania na makumbusho ya Mkoa Iringa Boma kama wadau wakubwa wa utalii Tanzania na nyanda za juu kusini tulipata nafasi ya kushiriki kwenye shughuli hii iliyo fanyika kwa mara ya kwanza Wilaya ya Tukuyu Mkoani Mbeya.

Mradi wa fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya mkoa unatoa shukrani na pongezi dhati kwa wote waliotembelea banda letu la maonesho kwa siku zote tulizo shiriki kwani ni moja kati ya kutngaza utalii wa nyanda za juu kusini.