Lindi Ni miongoni mwa mikoa inayopatikana Tanzania ni moja kati ya Mikoa mikongwe ilioanza kati ya karne ya 11 kwenye historia ya Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla. Historia ya Mkoa wa Lindi inapambwa na badhii ya maeneo yaliopo kwenye wilaya za Mkoa huo. Jina la Lindi maana yake ni SHIMO REFU, Bandari ya Lindi ilitumika katika kusafirishia watumwa kutoka Ziwa Nyasa. Waarabu waliofika karne ya 18, wahindi,wajerumani na waingereza ni miongoni mwa mataifa yaliyofanikiwa kuishi katika mkoa huu.

Mradii wa fahari yetu Tanzania na makumbusho ya Mkoa Iringa Boma tulifanikiwa kufika katika mkoa wa Lindi kwa ajili ya utafititi wa mambo kale na zana za asili zilizo tumika na wazawa tangu miaka 100 iliyopita. Lindi mjini, Kilwa Kipatimu (Nandete), Kilwa Kivinje, Kilwa Kisiwani Songo Mnara (Mji wa kale wa kiaarabu), Kilwa Masoko na Nchinga ni baadhi ya maeneo tuliyofanikiwa kuetembelea na kufanya utafiti katika mkoa wa Lindi.