Kuna mengi tuli jifunza hapa Kagera ikiwa ni pamoja na uhifadhi wa utamaduni wao hasa wa matumizi ya lugha ya asili, Pia tulipata fursa ya kufanya utafiti wetu kwa siku kadhaa kwenye falme za Buhaya chini ya watemi kama Mkama Kahigi,Mtemi Lukamba na Mtemi wa Karagwe.

Hata hivyo tulitembelea Makumbusho ya Kagera kujifunza na kujionea uhifadhi wa zana za kale zilizo hifadhiwa hadi leo.