Wizara ya Maliasili na Utalii Tanzania ili andaa maonesho na kutoa mialiko kwa wadau mbalimbali wa utalii, ikiwemo Mradi wa fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma, maonyesho haya yenye lengo la kuwajengea waheshimiwa wabunge uelewa na kuwapatia elimu kuhusu uhifadhi wa wanyamapori, malikale, na uendelezaji wa utalii nchini maonesho yalifanyika katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma kuanzaia tarehe 30 Mei hadi 3 Juni 2024.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angela Kairuki, alipotembelea banda la Makumbusho ya Mkoa wa Iringa Boma, alitoa pongezi za dhati kwa mradi wa fahari yetu Tanzania kwa juhudi kubwa wanazozifanya katika kutangaza na kuendeleza utalii wa kiutamaduni. Waziri Kairuki alisisitiza umuhimu wa mradi huu katika kuanzisha na kusimamia makumbusho ya Mkoa wa Iringa, jambo ambalo lina mchango mkubwa katika kuhifadhi na kuendeleza utamaduni wa taifa letu.

“Nimefurahishwa sana na kazi kubwa mnayofanya katika kutangaza utalii wa kiutamaduni,” alisema Waziri Kairuki. “Nimekuwa nikifuatilia taarifa zenu kupitia mitandao ya kijamii kama Instagram, na ni dhahiri kuwa mnachangia kwa kiasi kikubwa katika kuonyesha uzuri na utajiri wa utamaduni wetu kwa dunia nzima.”

Dkt. Jan Kuver, Mkurugenzi wa Mradi wa Fahari Yetu na makumbusho ya Iringa Boma, anaeleza kuwa, Maonyesho haya yaliyofanyika Dodoma ni jukwaa muhimu la kutangaza utalii wa ndani na nje kwa wabunge na wadau wengine wa utalii. Maonyesho haya yanaweza kuongeza chachu ya kutangaza utalii kwa kuwawezesha wabunge na viongozi wengine kuona na kushiriki moja kwa moja katika shughuli za utalii, na hivyo kuboresha uelewa na ushirikiano wao katika kuendeleza sekta hii muhimu. Ushirikiano baina ya Wizara ya Utalii na wadau wengine katika maonyesho haya ni wa manufaa makubwa, kwani unawawezesha kubadilishana mawazo na mbinu bora za kutangaza utalii, na hivyo kuleta ubunifu na ufanisi katika sekta hii.

“Kupitia maonyesho haya, sisi kama fahari fetu Tanzania tumejifunza vingi na kupata fursa ya kukutana na wadau wengi ambao tunaweza kushirikiana nao katika kufanya shughuli za utalii”.

Makumbusho ya mradi wa fahari yetu Tanzania unatoa  shukrani kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaliko huu muhimu.Kwani umetuwezesha kuelezea shughuli zinazofanywa na makumbusho na kutoa fursa ya kutangaza utalii kwa waheshimiwa wabunge. Tunatumaini kuwa wabunge hawa watakuwa mabalozi wa kutangaza utalii unaopatikana Iringa katika majimbo wanayowakilisha.

Maonesho ya pamoja ya Mradi wafahari yetu Tanzania na Kibubu Ufinyanzi yamefanyika kwa mafanikio makubwa katika viwanja vya Nafasi Art Space Mikocheni B jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Januari 2024. Mradi wa wafahari yetu Tanzania uliwasilisha maonesho ya “Endangered Story of Enchanted Place Phase II, huku Kibubu Ufinyanzi wakionyesha ubunifu wao katika kufinyanga vitu vyenye naumbo mbalimbali kwamatumizi ya  kuhifadhi fedha..

Maonesho haya yalikuwa ni matokeo ya ufadhili ambao waliipokea kutoka Nafasi Art Space mwaka mmoja uliopita. Dkt. Noel Lwoga, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maonesho haya, alitoa maoni yake akisema, “Ni vyema kutangaza utalii kwa njia tofauti”. Tumeona mradi wa wafahari Yetu Tanzania wameamua kuleta simulizi zilizomo katika jamii zetu. Simulizi hizi zenye kuibua hisia kwa watu, ingawa zinaweza kuonekana kama za kufikirika lakini nisimulizi zakweli na zenye kusisimua.

Mkurugenzi wa Nafasi Art Space aliongezea kwa kusema kuwa wamefurahi kuona mafanikio ya ufadhili waliotoa na kuwakaribisha wanasanaa wengine kuomba ufadhili. Hama hivyo. Dkt. Jan Kuver, Meneja wa mradi wa fahari yetu Tanzania, alielezea kuwa maonesho haya yalikuwa ya pili, baada ya yale yaawali kufanyika Iringa na sasa yamehamishiwa Dar es Salaam. Pia, wanaendelea kuandaa vitabu vyenye picha za kuchora kwa ajili ya kusambaza mashuleni ili kuendelea kuhifazi msimulizi haya kupitia kwa watoto.

Maonesho haya yamekuwa ni fursa nzuri ya kukuza utamaduni, ubunifu, na kuelimisha jamii kuhusu mambo mbalimbali yanayowahusu. Tunatarajia kuona juhudi kama hizi zikiendelea na kuchochea maendeleo katika sekta za utalii na sanaa nchini Tanzania.

Maonesho ya pamoja ya Mradi wafahari yetu Tanzania na Kibubu Ufinyanzi yamefanyika kwa mafanikio makubwa katika viwanja vya Nafasi Art Space Mikocheni B jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Januari 2024. Mradi wa wafahari yetu Tanzania uliwasilisha maonesho ya “Endangered Story of Enchanted Place Phase II, huku Kibubu Ufinyanzi wakionyesha ubunifu wao katika kufinyanga vitu vyenye naumbo mbalimbali kwamatumizi ya  kuhifadhi fedha..

Maonesho haya yalikuwa ni matokeo ya ufadhili ambao waliipokea kutoka Nafasi Art Space mwaka mmoja uliopita. Dkt. Noel Lwoga, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maonesho haya, alitoa maoni yake akisema, “Ni vyema kutangaza utalii kwa njia tofauti”. Tumeona mradi wa wafahari Yetu Tanzania wameamua kuleta simulizi zilizomo katika jamii zetu. Simulizi hizi zenye kuibua hisia kwa watu, ingawa zinaweza kuonekana kama za kufikirika lakini nisimulizi zakweli na zenye kusisimua.

Mkurugenzi wa Nafasi Art Space aliongezea kwa kusema kuwa wamefurahi kuona mafanikio ya ufadhili waliotoa na kuwakaribisha wanasanaa wengine kuomba ufadhili. Hama hivyo. Dkt. Jan Kuver, Meneja wa mradi wa fahari yetu Tanzania, alielezea kuwa maonesho haya yalikuwa ya pili, baada ya yale yaawali kufanyika Iringa na sasa yamehamishiwa Dar es Salaam. Pia, wanaendelea kuandaa vitabu vyenye picha za kuchora kwa ajili ya kusambaza mashuleni ili kuendelea kuhifazi msimulizi haya kupitia kwa watoto.

Maonesho haya yamekuwa ni fursa nzuri ya kukuza utamaduni, ubunifu, na kuelimisha jamii kuhusu mambo mbalimbali yanayowahusu. Tunatarajia kuona juhudi kama hizi zikiendelea na kuchochea maendeleo katika sekta za utalii na sanaa nchini Tanzania.

 

“Karibuni sana wageni kuwekeza katika Utalii wa Tanzania, inawezekana ukawekeza katika utalii wa chakula, utalii wa kiutamaduni lakini pia utalii wakupokea wageni majumbani (Home Stay Tourism) Lengo letu ni kuhakikisha tuna kuza na kutangaza utalii wa Tanzania kwa njia yoyote ile” Mhe. Angela Kairuki Waziri wa maliasili na Utalii Tanzania. ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa maonesho ya Swahili International Expro yaliyofanyika jijini Dar es laam.

Mr.Jimson sanaga Meneja mwenza mradi wa fahari yetu Tanzania na makumbusho ya mkoa Iringa boma anasema ni mara yao ya nne sasa kuhudhuria katika maonesho hayo makubwa ya utalii Tanzania, na kila mwaka maonesho hayoyamekuwa yakiutofauti.

“Kwa miaka yote minne ambayo tumehudhuria katika maonesho haya tumeona utofauti mkubwa sana, maonesho yametusaidia katika kutangaza utalii wetu wa Tanzania na hususa ni utalii wa nyanda za juu kusini” hata hivyo bado tunanafasi kubwa sana yakuendelea kutangaza utaklii wandani na hata wakuhistoria ameongeza Mr. Sanga yakuwa mradi wafahari yetu kwasasa upo kwenye utafiti wa masimulizi ya kale yaliyo hatiani kupotea kwa lengo la kuyakusanya na kuyahifadhi kwa jili ya vizazi vijavyo.

Maonesho ya Swahili International Tourism Expro (S!TE) hufanyika kila mwaka nchini Tanzania, maonesho haya yanalengo la kukutanisha wadau mbalimbali wa utalii wandani ya nchi na nnje ya nchi kwalengo la . Kwamwaka wa 2023 maonesho haya yamefanyika kuanzania tarehe 6 hadi mwezi wa 10 katika viwanja wa mlimani City jijini Dar es Laam.

 

 

Je! unatafuta eneo sahihi kwa ajili ya kufanya biashara ya Mgahawa, ndio pengine hujui wapi panaweza kuwa eneo sahihi zaidi, acha nikufahamishe yakuwa Makumbusho ya mkoa Iringa Boma inakutangazia kuwa inapangisha eneo lake la mgahawa kwa Muwekezaji aliye tayari.

Kuna kila sababu za kuwekeza katika eneo hili .

1.Eneo lipo katikati ya mji wa Iringa (Iringa Boma ) ilipokuwa ofisi ya mkuu wa Wilaya.

2. Nisehemu nzuri yenye muingiliano wa wageni kutoka nchi mbalimbali kutokana uwepo wa Makumbusho ya Mkoa.

3. Ulinzi na usalama ni wa hali ya juu.

Unasubiri nini sasa kwa mawasiliano zaidi tupigie kupitia

+255 753 975 333
+255 762 424 642

 

 

 

Sikukuu ya Sabasaba, inayojulikana pia kama Saba Saba Day, ni sikukuu ya kitaifa nchini Tanzania inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 7 Julai.

Sikukuu ya Sabasaba imekuwa muhimu katika kuimarisha umoja na mshikamano wa Watanzania na kuadhimisha historia ya taifa. Pia, inatoa fursa kwa wafanyabiashara na wajasiriamali kuonyesha bidhaa na huduma zao na kujenga uhusiano na wateja wapya.

Kwa mkoa wa Iringa sikukuu hii inaadhimishwa katika kijiji cha Pawaga ambapo mradi wa fahari yetu Tanzania na Makumbusho ya Mkoa Iringa Boma wamedhamini Mashindano ya ngoma za Asili na kutoa zawadi za jezi kwa washiriki waliyofanikiwa kuingia hatua ya robo fainali katikla michuano ya sababa.

Akizungumza na wananchi Mkuu wa wilaya wa Iringa amabaye alikuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa wiki ya sabasaba anasema watu wengi wanasahau asili yao kutokana na mabadiliko ya kiutandawazi hivyo amepongeza juhudi zinazofanywa na mradi wa fahari yetu Tanzania katika kuendeleza na kuenzi utamaduni kwakudhamini mashindano hayo.

Naye mkurugenzi mradi wa fahari yetu Tanzania Dr.Jan Kuever ameeleza kuwa mradi wa fahari yetu umekuwa ukijihusisha na kukuza,kutangaza na kuendeleza shughuli za kiutamaduni tangu kuanzishwa kwake.

It seems we can’t find what you’re looking for. Perhaps searching can help.